ROSE NDAUKA AKATAA KUMSAMEHE MZAZI MWENZAKE


Kama Bado Hujajiunga Nasi, Unaweza Kujiunga Hapa Nikutumie Habari Moja Kwa Moja ..Bofya HAPA ULIKE PAGE YETU!..

Diva wa filamu Bongo, Rose Ndauka akiwa na mzazi mwenziye, Malick Bandawe.
Na Laurent Samatta/Amani
DIVA wa filamu Bongo, Rose Ndauka ametoa ya rohoni kwamba hatokaa amsamehe mzazi mwenziye, Malick Bandawe.
Akizungumza na Amani, Ndauka alisema alishawahi kufuatwa na mzazi mwenzake huyo kwa lengo la kumuomba msamaha ili waendelee na mapenzi yao lakini hakuwa tayari kumsamehe.
“Kuachana tumeshaachana, kama kurudi huwa inatokea lakini kwangu sipo tayari tena kumsamehe, anaweza kutokea mtu mwingine wa kunipenda ingawa kwa sasa nahitaji kupumzika kwanza,” alisema Rose.
Rose na mzazi mwenzake waliachana mwaka jana huku wakificha sababu za kuachana kwao.

0 comments:

Copyright © 2013. MAPYATZBLOG - All Rights Reserved
Customized by: MAPYATZBLOG | Powered by: http://bongoswagzs.blogspot.com/
Designed by: http://bongoswagzs.blogspot.com//