MWANAMITINDO FLAVIANA MATATA ACHUMBIWA NA MBONGO..ASEMA HAYA


Mwanamitindo Mtanzania Flaviana matata ambaye Novemba 2014 alichumbiwa, amesema kuwa hata atakapoolewa, ndoa haitabadilisha au kuathiri chochote katika kazi zake.
Flaviana Matata
“Kila kitu kitaendelea kama kilivyo sasa mpaka pale nitakapoona sasa imetosha nifanye mambo mengine, lakini haitabadilisha chochote, itabadilisha status tu ndo inakuwa mrs flani basi.” Alisema kupitia XXL ya Clouds Fm.
 
Mwanamitindo huyo wa kimataifa ambaye hufanyia shughuli zake Marekani, hajataka kumuweka wazi mchumba wake lakini amesema ni Mtanzania anayeishi Marekani.
 
Baada ya kuulizwa kwanini amechagua kuolewa na Mtanzania mwenzake, alijibu hiki:
 
“Utamaduni ni muhimu sana, Kiukweli simzui mtu kuolewa na utamaduni wowote lakini mimi najua nachokihitaji katika maisha yangu, najua hatufanani najua mwingine anataka mzungu mwingine muhindi, lakini mimi cha kwanza kabisa utamaduni ni muhimu sana.”


0 comments:

Copyright © 2013. MAPYATZBLOG - All Rights Reserved
Customized by: MAPYATZBLOG | Powered by: http://bongoswagzs.blogspot.com/
Designed by: http://bongoswagzs.blogspot.com//